WFP yasema imemaliza akiba yake ya chakula Gaza
25 Aprili 2025Matangazo
Katika taarifa, mkurugenzi wa WFP kwa Palestina Antoine Renard, amesema kuwa leo, shirika hilo limesambaza akiba yake ya mwisho ya chakula kwa maeneo yanayopika chakula kwa ajili ya wakazi wa eneo hilo la Gaza.
Mashirika ya kimataifa yaonya juu ya kitisho cha njaa zaidi
Renard ameongeza kusema kuwa uzuwiaji huo umeendelea kwa zaidi ya siku 50 na ikiwa hali itaendelea kuwa vilevile, msaada wa dharura wa WFP huenda ukalazimika kusitishwa..
WFP lasitisha harakati Ukanda wa Gaza
Baada ya miezi 18 ya vita, shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kiutu OCHA lilisema Jumanne kwamba hali katika ukanda wa Gaza huenda ikawa sasa ndio mbaya zaidi.