WFP: Wakimbizi wa Sudan wako hatarini kukabiliwa na njaa
30 Juni 2025WFP imesema hayo yanaweza kutokea hasa wakati huu kukishuhudiwa upungufu wa ufadhili wa msaada wa chakula.
Shaun Hughes, mratibu wa masuala ya dharura wa WFP huko Sudan amesema mgogoro huu ambao ni wa kikanda, unashuhudiwa katika nchi ambazo tayari zina viwango vya juu vya mizozo na uhaba wa chakula. Shirika hilo limetahadharisha kuwa msaada kwa wakimbizi wa Sudan walioko Misri, Ethiopia, Libya na Jamhuri ya Afrika ya Kati huenda ukasitishwa katika miezi ijayo kutokana na ukosefu wa ufadhili.
Tangu Aprili mwaka 2023, vita kati ya jeshi la Sudan na wapiganaji wa kundi la RSF vimesababisha mzozo mkubwa zaidi wa wakimbizi duniani, huku zaidi ya watu milioni 10 wakiwa wakimbizi wa ndani na wengine milioni nne wakikimbilia nje ya nchi hasa katika mataifa ya Chad, Misri na Sudan Kusini.