JangaKimataifa
WFP: Kupungua ufadhili kwa 40% kunahatarisha maisha duniani
28 Machi 2025Matangazo
Hayo ni kutokana na kupungua kwa ufadhili kwa shirika hilo kwa asilimia 40 na kuhatarisha maisha ya watu milioni 58.
WFP imeongeza kwamba licha ya jitihada kubwa kutoka kwa serikali mbalimbali na watu binafsi duniani kote, bado shirika hilo linakabiliwa na kushuka kwa ufadhili kutoka kwa wafadhili wake wakuu.
Miongoni mwa operesheni muhimu za shirika hilo zinazokabiliwa na kitisho hicho ni pamoja na zile zilizopo katika mataifa ya Afrika Mashariki kama Kenya, Somalia, Burundi, Sudan Kusini, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Hapo jana WFP ilionya kwamba imebakiwa na chakula cha wiki mbili pekee huko Gaza, ambapo "mamia ya maelfu ya watu" wako katika hatari ya njaa kali na utapiamlo.