Waziri Wadephul wa Ujerumani ziarani Mashariki ya Kati
1 Agosti 2025Matangazo
Baada ya kukutana na viongozi wa Israel mjini Jerusalem siku ya Alhamisi, Wadephul anapanga kusafiri kwenda katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kimabavu na Israel ambapo atakutana mjini Ramallah na Rais wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas.
Wadephul na Abbas watajadili suala la ghasia zinazoendeshwa na walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi pamoja na majadiliano yanayoendelea Israel kuhusu uwezekano wa kulinyakua eneo hilo.