JamiiItaly
Waziri Mkuu wa Italia Meloni amtembelea Papa hospitalini
20 Februari 2025Matangazo
Meloni alimtembelea Papa kwa dakika 20 jana Jumatano na kusema alionekana mwenye nafuu na mcheshi, licha ya kugundulika na maradhi hayo, ambayo yamemuweka hosptalini kwa siku sita.
Kulingana na ofisi ya Meloni, kiongozi huyo alitaka kupeleka salamu za heri kwa papa kwa niaba ya serikali na taifa zima.
Meloni amekuwa mgeni wa kwanza aliyethibitishwa kutoka nje aliyemtembelea Papa Francis. Tofauti na yeye, Kiongozi huyo wa juu kabisa wa Kanisa Katoliki hukutana na wasaidizi na madaktari wake tangu alipolazwa siku ya Ijumaa katika hospitali ya Gemelli, mjini Rome.