Netanyahu na Trump kukutana kwa mazungumzo Washington
4 Februari 2025Matangazo
Netanyahu anayekuwa kiongozi wa kwanza wa kigeni kuizuru Ikulu ya White House tangu Trump aliporejea madarakani mwezi uliopita, atajadiliana naye kuhusu mustakabali wa makubaliano hayo pamoja na jitihada za kuvimaliza vita katika Ukanda wa Gaza.
Netanyahu kujadili na Trump "ushindi dhidi ya Hamas" na Iran
Saa chache kabla ya mkutano huo, ofisi ya Netanyahu ilisema Israel itapeleka ujumbe mjini Doha, Qatar baadae wiki hii kwa ajili ya mazungumzo.
Kundi la Hamas limesema liko tayari kujadili hatua ya pili ya usitishaji huo wa mapigano unaosimamiwa na Qatar, Misri na Marekani.