Netanyahu asema Hamas imekiuka makubaliano
21 Februari 2025Matangazo
Netanyahu amesema Israel itafanya juhudi zote kuurejesha mwili wa Shiri nyumbani.
"Tutafanya kazi kwa dhamira ya kumleta Shiri nyumbani pamoja na mateka wetu wote, walio hai na waliokufa, na kuhakikisha kuwa Hamas inalipia kikamilifu ukiukaji huu wa kikatili na wenye nia mbaya wa makubaliano,alisema Netanyahu."
Kumbukumbu takatifu ya Oded Lifshitz na Ariel na Kfir Bibas itakuwa daima kwenye moyo wa taifa. Mungu awalipizie damu yao. Sisi pia tutalipiza.
Netanyahu: Ninaunga mkono mpango wa Trump kwa Gaza
Huku miili ya watoto wa kiume wa Bibas na mateka mmoja mzee ikitambuliwa na wataalamu wa uchunguzi wa maiti wa Israel, kulingana na maafisa wa Israel, mwili wa nne haukuwa wa Shiri Bibas, kama inavyodaiwa na Hamas.