Waziri mkuu wa Australia apuuza shtuma za Netanyahu
20 Agosti 2025Matangazo
Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Albanese amesema hayachukulii masuala hayo kwa uzito na kwamba anashirikiana na watu kidiplomasia.
Wakati huo huo, waziri wa mambo ya ndani waAustraliaTony Burke, mapema leo, ameliambia shirika la habari la serikali ABC kwamba nguvu haipimwi kwa idadi ya watu unaoweza kulipua ama idadi ya watoto unaoweza kuwaacha njaa.
Albanese asema Netanyahu anafumbia macho hali halisi ya Gaza
Burke amesema kuwa nguvu inapimwa vizuri zaidi na kile alichokifanya Albanese, ambapo panapokuwa na uamuzi ambao wanafahamu Israel haitaridhia, anakwenda moja kwa moja kwa Nentanyahu.