MigogoroMashariki ya Kati
Hamas waelekea Uturuki kujadili mazungumzo yaliyokwama Doha
29 Julai 2025Matangazo
Chanzo kutoka kundi hilo kimesema ujumbe wa Hamas umeongozwa na Rais wa Baraza la uongozi wa kundi hilo Mohammed Darwish pamoja na mkuu wa usuluhishi Khalil al-Hayya.
Chanzo hicho kimesema timu hiyo itashiriki mikutano kadhaa na maafisa wa Uturuki kujadili yaliyojitokeza kwenye mazungumzo ya Doha yaliyokwama wiki iliyopita. Kwa majuma mawili, wasuluhishi nchini Qatar walikuwa wakihangaika kupata muafaka ili kusitisha mapigano.
Marekani iliungana na Israel kuwaondoa wasuluhishi wake kwenye majadiliano hayo. Mwakilishi wa Marekani katika eneo la Mashariki ya kati Steve Witkoff alililaumu kundi la Hamas kwa kushindwa kufikia makubaliano.