UchumiChina
China, US zajadili namna ya kutuliza mvutano wa kibiashara
10 Mei 2025Matangazo
Mvutano kati ya China na Marekani ulisababisha pia mparaganyiko kwenye uchumi wa dunia. China imewakilishwa na Naibu Waziri Mkuu He Lipeng huku Marekani ikiwakilishwa na Waziri wake wa Fedha Scott Bessent.
Hata hivyo kuna matarajio hafifu kwamba mazungumzo hayo yatafikia mafanikio makubwa huku kukiwa na hali ya kutoaminiana kati ya Washington na Beijing.
Soma pia: Shirika la WTO lapongeza mazungumzo ya kibiashara kati ya Marekani na China
Vita hivyo vya kibiashara vilichochewa na hatua ya mwezi uliopita ya Rais wa Marekani Donald Trump kuyawekea ushuru mkubwa mataifa kadhaa ulimwenguni na hivyo kuvuruga minyororo ya ugavi, ustawi wa masoko na kuzusha hofu ya kuzorota kwa ukuaji wa uchumi kote duniani.