MigogoroMashariki ya Kati
Watu 28 wauawa kutokana na mashambulizi ya Israel huko Gaza
23 Mei 2025Matangazo
Jeshi la Israel linaendelea na mashambulizi yake na limetangaza kwamba operesheni zake dhidi ya makundi ya kigaidi zitaendelea kote katika Ukanda wa Gaza.
Taarifa ya jeshi la Israel imesema magaidi kadhaa wameuliwa na kwamba jeshi limeharibu kambi za kijeshi, silaha na maeneo ya kuhifadhia vifaa vya kijeshi. Madai hayo hayakuweza kuthibitishwa na duru zisizotegemea upande wowote.
Vita vya Gaza vilichochewa na shambulio baya la kigaidi lililofanywa na Hamas na wanamgambo wengine nchini Israeli mnamo Oktoba 7, 2023. Mamlaka ya afya inayodhibitiwa na Hamas ilisema vita hivyo vimewauwa zaidi ya Wapalestina 53,000.