JangaUlaya
Watu watatu wafariki Ulaya kufuatia mioto ya nyika
13 Agosti 2025Matangazo
Watu wawili walifariki huko Uhispania na mmoja nchini Montenegro. Tahadhari ya hali ya joto la kupindukia imetolewa katika mataifa ya Italia, Ufaransa, Uhispania, Ureno na nchi za Balkan, ambako joto linatarajiwa kufikia hadi nyuzijoto 40 katika kipimo cha Celsius.
Akshay Deoras, mtafiti katika idara ya hali ya hewa katika Chuo Kikuu cha Reading nchini Uingereza amesema hali hiyo ya joto kali ni ishara nyingine ya mabadiliko ya hali ya hewa lakini bado watu wengi hawatilii maanani hatari hiyo inayotukabili.