Watu wamiminika Vatican kumuaga Papa Francis
22 Aprili 2025Salamu za rambirambi zinaendelea kutolewa kutoka kote ulimwenguni, huku makadinali wanaokutana Vatican wakiendeleza mipango ya mazishi yake pamoja na kuanzisha mchakato wa kumchagua mrithi wake.
Viongozi wa dunia wajiandaa kushiriki mazishi ya Papa Francis
Katika taarifa yake, Vatican imesema kuwa watu wataweza kutoa heshima zao za mwisho kwa Papa Francis papa wa kwanza kutoka Amerika ya Kusini, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Peter kuanzia Jumatano hadi Ijumaa.
Mwili wa Papa Francis kuwekwa kanisa la Mtakatifu Marta
Siku ya Jumatano, watu wataruhusiwa kutoa heshima zao za mwisho kuanzia saa tano asubuhi majira ya Vaticanhadi saa sita usiku.
Alhamisi kuanzia saa moja asubuhi hadi saa sita usiku na Ijumaa kuanzia saa moja asubuhi hadi saa moja usiku.