JamiiMarekani
Watu kadhaa wahofiwa kufa katika ajali ya ajali ya ndege
30 Januari 2025Matangazo
Ndege hiyo aina ya Bombardier CRJ ya kampuni ya American Airlines ilikuwa imewabeba abiria 60 na wafanyakazi wanne na ilikuwa inakaribia kutua kwenye uwanja wa ndege wa Reagan Washington pale ilipogongana na helikopta ya kijeshi.
Maafisa bado hawajatoa idadi ya watu waliokufa, lakini Seneta wa jimbo la Kansas eneo ambako ndege hiyo ilianzia safari ameashiria kwamba huenda abiria wengi au wote walikuwamo wamepoteza maisha.
Kituo cha televisheni cha CBS kikimnukuu afisa mmoja wa polisi kimeripoti kwamba miili isiyopungua 18 tayari imeopolewa kutoka Mto Potomac ambamo ndege hiyo ilianguka.