Sheria na HakiUlaya
Watu kadhaa wakamatwa juu ya sakata la rushwa bunge la Ulaya
13 Machi 2025Matangazo
Waendesha mashataka wamesema, kwamba takriban maafisa 100 wa polisi wa shirikisho waliendesha msako katika maeneo 21 mjini Brussels, katika mikoa ya Waflemish na Walonia pamoja na nchini Ureno.
Washukiwa waliokamatwa watahojiwa kuhusiana na tuhuma za kuhusishwa kwao na ulaji rushwa katika bunge la Ulaya,pamoja na tuhuma za kuendesha shughuli za kughushi nyaraka.
Soma pia:Umoja wa Ulaya washinikizwa kukatiza msaada kwa Rwanda
Taarifa za vyombo vya habari zinasema kwamba kampuni ya Kichina ya Huawei imekuwa ikiwapa rushwa wabunge wa bunge la Ulaya ili kuisadia kutangaza sera yake ya kibiashara barani Ulaya.