MigogoroYemen
Watu 8 wauawa Yemen kufuatia mashambulizi ya Marekani
28 Aprili 2025Matangazo
Hayo yameelezwa na kituo cha televisheni cha Al-Massira kinachodhibitiwa na waasi hao,na kusisitiza kuwa wanawake na watoto ni miongoni mwa waliouawa eneo la Thaqban katika mkoa wa Bani Al-Har, kaskazini mwa mji wa Sanaa.
Jeshi la Marekani limesema siku ya Jumapili kuwa kuanzia Machi 15 mwaka huu, limeyashambulia maeneo 800 nchini Yemen na kuua mamia ya Wahouthi.
Waasi wa Kihouthi wa Yemen wamekuwa wakizishambulia meli za kimataifa zinazopita katika bahari ya Shamu, kama ishara ya kuwaunga mkono wanamgambo wa Hamas katika vita vyao na Israel huko Gaza.